Masaa Arobaini na Nane Katika Jehanamu

Imeandikwa na John Reynolds

Mojawapo ya mifano iliyohai na ya kuvutia kabisa ya kurudishiwa uhai wa mtu aliyekwisha kufa ambayo imewahi kuja kwa ufahamu wangu ulikuwa ni ule wa George Lennox, mwizi stadi wa farasi kutoka Jimbo la Jefferson (Marekani). Alikuwa akitumikia kifungo chake cha pili. Jimbo la Sedwick lilimpeleka gerezani kwa mara ya kwanza kwa kosa hilo hilo – wizi wa farasi. 

Wakati wa majira ya baridi ya mwaka 1887 na 1888 alifanya kazi kwenye machimbo ya makaa ya mawe. Mahali alipokuwa akifanyia kazi palionekana kwake kuwa ni pa hatari. Hivyo, alitoa taarifa ya jambo hili kwa ofisa aliyehusika, ambaye alifanya uchunguzi, na baada ya kuamua kuwa chumba hicho kilikuwa ni salama alimwamuru Lennox arudi kwenye kazi yake. Basi mfungwa, akitii, alikuwa hajafanya kazi yake kwa zaidi ya saa moja, wakati sakafu ya juu ikaanguka chini ghafla na kumzika kabisa. Alibakia katika hali hii kwa masaa mawili kamili.

Alipokosekana wakati wa chakula cha mchana, msako ulifanywa kwa ajili ya mfungwa huyu, na alipatikana chini ya kifusi hiki cha udongo. Uhai ulionekana umemtoka. Alipelekwa hadi juu, na baada ya kufanyiwa uchunguzi na daktari wa jela, alitangazwa kwamba alikuwa ameshafariki. Mabaki yake yalichukuliwa hadi hospitalini ambapo alioshwa na kuvishwa, kabla ya mazishi. Jeneza lake lilitengenezwa na kuletwa hospitalini. Mchungaji wa gereza alikuwa amefika kuendesha ibada ya mwisho ya kuhuzunisha kabla ya mazishi. Wafungwa wawili waliamriwa na msimamizi wa hospitali kuinua marehemu kutoka kwenye mbao na kumbeba, kwa kupita katikati ya chumba na kuiweka ndani ya jeneza. Walitii, mmoja akishika kichwani na mwingine miguuni na walikuwa karibu kufika katikati ya chumba, wakati yule ambaye alikuwa kichani alijikwaa kwa bahati mbaya kwenye chungu cha maua, akayumba, na kudondosha maiti. Kichwa cha marehemu kilijigonga kwenye sakafu, na kwa mshangao mkubwa na wa kustaajabisha kwa wote waliokuwepo, sauti kubwa ya mlio wa maumivu ilisikika. Mara macho yalifumbuka na dalili nyingine za uhai zilijionyesha. Daktari aliitwa mara moja, na baada ya kufika, kama dakika thelathini, mtu aliyekufa alikuwa ameomba kikombe cha maji, na alikuwa katika tendo la kunywa wakati daktari alipowasili. Jeneza liliondolewa mara moja na lilitumika baadaye kumzikia mfungwa mwingine. Nguo zake alizovalishwa kwa ajili ya mazishi zilichukuliwa pia kutoka kwake na kuvalishwa badala yake vazi maalum la gereza. Katika kumfanyia uchunguzi alionekana kuwa mguu wake mmoja ulikuwa umvunjika katika sehemu mbili, na vinginevyo ulichubuliwa. Alibakia hospitalini kama miezi sita, na akarudia tena kufanya kazi.

Nilijifunza kuhusu hali yake ya ajabu aliyopitia wakati akiwa amekufa muda mfupi tu baada ya hapo, kutoka kwa mchimba makaa mwenzake. Nikisukumwa kwa udadisi, nilitamani kukutana na Lennox ili nisikie hali yake aliyopitia kutoka mdomoni mwake; nafasi hii ilikosekana kwa miezi  mingi. Hatimaye ilikuja. Baada ya kutolewa kutoka kwenye machimbo ya makaa ya mawe nilipangiwa kwenye mojawapo ya ofisi ya jela kutayarisha baadhi ya taarifa za mwaka. Suala la mtu huyu kufufuka tena lilikuwa likizungumzwa siku moja, akiwa akipita karibu na mlango wa ofisi na alionyeshwa kwangu. Haikuchukua muda hadi nilipompa karatasi kidogo mkononi mwake ya kumwomba aje mahali nilipokuwa nikifanya kazi. Alikuja, na hapo nilifahamiana naye vizuri, na kutoka midomoni mwake mwenyewe nilipata habari zake za ajabu. Yeye ni kijana, hawezi kuzidi umri wa miaka thelathini. Alikuwa ni mhalifu mzoefu; na alikuwa na elimu nzuri sana na hivyo mwenye akili sana.

Sehemu ya kustaajabisha kabisa ya habari zake zilikuwa ni ule wakati alipokuwa amekufa. Nikiwa mwanandishi wa habari, nilichukua habari zake kutokana na maneno yake.

Maandiko kamili ya: Masaa Arobaini na Nane Katika Jehanamu

Alisema; “Asubuhi yote nilikuwa na hofu ya kuwa jambo fulani la kutisha lingetokea. Sikujisikia vizuri katika hali yangu kiasi kwamba nilimwendea mkubwa wangu wa machimbo ya makaa, Bwana Grason, na kumwambia jinsi nilivyojisikia, na kumwomba aje na kufanya uchunguzi wa chumba changu cha makaa, mahali ambapo nilikuwa nikichimba makaa ya mawe. Alikuja  na alionekana kufanya uchunguzi thabiti, na aliniamuru kurudi, akisema hapakuwa na hatari na kwamba alidhani nilikuwa nikirukwa na akili! Nilirudi kazini kwangu, na nilikuwa katika kuchimbua kwa kadri ya saa moja, wakati ghafla ilikuwa giza kabisa, kisha ikaonekana kwamba lango kubwa  la chuma lilijifungua na nilipita katikati yake. Baadaye wazo lilinijia akilini mwangu kwamba nilikuwa nimekufa na niko katika ulimwengu mwingine. Sikuweza kumwona  mtu yeyote wala kusikia sauti ya aina yoyote. Kutokana na sababu ambayo mimi mwenyewe sikuifahamu, nilianza kuondoka kutoka kwenye lile lango wazi, na nilikuwa nimesafiri umbali fulani wakati nilipofika kwenye kingo za mto mpana. Haikuwa giza wala hapakuwepo na nuru. Kulikuwepo na mwangaza wa kutosha kama ilivyo katika usiku ulioangazwa kwa nyota. Nilikuwa sijabakia kwenye kingo za mto huu kwa muda mrefu wakati niliposikia sauti ya makasia ya mtumbwi majini, na mara mtu akiwa mtumbwini, akipiga makasia kuelekea mahali nilipokuwa nikisimama.

“Sikuweza kuzungumza neno. Aliniangalia kwa kitambo, na kisha alisema kwamba alikuwa amenijia mimi, na aliniambia kuingia mtumbwini na kuvuka hadi upande mwingine. Nilitii. Sikusema hata neno moja. Nilitamani kumwuliza kuwa yeye ni nani, na nilikuwa wapi. Ulimi wangu ulionekana kung’ania kwenye sehemu ya juu ya kinywa changu. Hivyo sikuweza kusema neno. Hatimaye, tulifikia ng’ambo ya pili. Nilitoka nje ya mtumbwi, na mpiga makasia ya mtumbwi alitoweka ghafla mbele ya macho yangu!

“Hivyo, nikiwa nimeachwa peke yangu, sikujua nifanye nini. Nikiangalia mbele yangu, niliona barabara mbili ambazo ziliongoza hadi kwenye bonde lenye giza. Mojawapo ya hizi, ilikuwa ni barabara pana na ilionekana kuwa inapitika sana. Nyingine ilikuwa ni njia nyembamba na ilielekea upande mwingine. Bila ya kufahamu, nilifuata barabara pana iliyokanyagwa sana. Nilikuwa sijaenda mbali wakati kulipoongezeka kuwa giza zaidi. Lakini kila baada ya muda, nuru iliweza kuangaza kutoka kwa mbali, na kwa jinsi hii niliweza kuendelea katika safari yangu.

 “Punde kidogo nililakiwa na kiumbe ambacho ni vigumu kabisa kwangu kukielezea. Ninaweza tu kukupa picha hafifu ya sura yake ya kuogofya. Alifanana na mtu kwa kiasi fulani, lakini alikuwa mkubwa zaidi kuliko mwanadamu yeyote ambaye niliwahi kumwona. Alikuwa siyo chini ya mita tatu kwa urefu wa kwenda juu. Alikuwa na mabawa makubwa mgongoni mwake. Alikuwa ni mweusi kama mkaa niliokuwa nikichimba, na alikuwa katika hali ya uchi kabisa. Alikuwa na mkuki mkononi mwake, ambao mpini wake ni lazima ulikuwa mita tano kwa urefu. Macho yake yaliwaka kama goroli za moto. Meno yake, meupe kama lulu, yalionekana kuwa inchi moja kwa urefu. Pua yake (ikiwa unaweza kuiita pua), ilikuwa kubwa sana, pana na bapa. Nywele zake zilikuwa ni za singa, nzito na ndefu. Zilitua juu ya mabega yake makubwa. Sauti yake ilisikika zaidi kama ngurumo za simba aliyeko kwenye zizi la wanyama kuliko kitu chochote ninachoweza kukikumbuka.

“Ilikuwa ni katika mmojawapo wa mimuliko hii ya nuru iliyoniangazia njia kwamba nilimwona kwa mara ya kwanza. Nilitetemeka kama jani nilipomwona. Alikuwa amenyanyua mkuki wake kama alitaka kunirushia. Ghafla nilisimama. Kwa sauti ile ya kutisha alinisihi nimfuate. Nikamwandama. Ningefanya jambo gani jingine? Baada ya kuwa amekwenda umbali fulani mlima mkubwa ulionekana kuinuka  mbele yetu. Sehemu iliyo mbele yetu ilionekana kusimama wima, kama vile mlima ulikuwa umekatwa katikati, na sehemu moja ilikuwa imechukuliwa. Juu ya ukuta huu uliosimama wima niliweza kuona kwa wazi kabisa maneno haya ‘Hii ni Jehanamu!’. Kiongozi wangu aliukaribia ukuta huu wima, na kwa mpini wake wa mkuki aligonga kwa sauti mara tatu. Lango kubwa tena zito lilifunguka na tuliingia ndani. Kisha niliongozwa kupita katika ile ambayo ilionekana kama ni njia ya ndani kwa ndani katika mlima huu.

“Kwa muda kadhaa tulisafiri katika giza nene. Niliweza kusikia vishindo vizito vya miguu ya kiongozi wangu na hivyo kuweza kumfuata. Katika njia yote niliweza kusikia sauti za mikoromo mizito kama ile ya mtu anayekufa. Mbele zaidi, mikoromo hii iliongezeka, na niliweza kusikia kwa wazi kabisa vilio vya ‘maji, maji, maji.’ Nikija sasa kwenye lango jingine, na kulipitia, niliweza kusikia mamilioni ya sauti kwa mbali, na mwito ulikuwa ni ‘MAJI.’ Punde kidogo lango jingine kubwa lilifunguka kutokana na kugonga kwa kiongozi wangu, na nilitambua kwamba tulikuwa tumekwisha pita ndani ya mlima, na sasa uwanda mpana ulikuwa mbele yetu.

 “Kwa mahali hapa kiongozi wangu aliniacha kwenda kuongoza roho zingine zilizopotea kuja mahali hapa. Nilibakia kwenye uwanda huu ulio wazi kwa muda, wakati kiumbe kilichofanana na kile cha kwanza kiliponijia; ila badala ya mkuki alikuwa na upanga mkubwa. Alikuja kuniambia kuhusu hukumu yangu ya baadaye. Alizungumza kwa sauti ambayo ilileta kitisho rohoni mwangu. ‘Uko katika Jehanamu’, alisema: ‘kwako wewe matumaini yote yametoweka. Ulipopita ndani ya mlima ukiwa njiani kuja hapa, ulisikia mikoromo na sauti zikilia kutokana na maumivu ya wale waliopotea walipokuwa wakiomba maji ya kupoza ndimi zao zilizokauka. Katika njia hiyo ndani ya mlima kuna mlango ambao unafungukia kwenye ziwa la moto. Muda sio mrefu hilo ndilo litakuwa hukumu yako. Kabla hujaongozwa hadi mahali hapo pa mateso ambapo hakuna kutoka tena – kwa kuwa hakuna tumaini kwa ajili ya wale ambao wameingia humo – utaruhusiwa kubakia kwenye uwanda huu wazi, ambako wapotevu wote wanapewa muda kwa kuangalia kile ambacho wangefurahia badala ya kile ambacho watateswa nacho.’

“Kwa maneno hayo, niliachwa peke yangu. Sijui kama ilikuwa ni matokeo ya hofu kubwa ambayo nilikuwa nimepitia, lakini sasa nilishikwa na bumbuazi. Hali ya kuishiwa kabisa nguvu iliushika mwili wangu. Nguvu yangu iliniacha. Miguu yangu haikuweza tena kuvumilia uzito wa mwili wangu. Nikiwa nimechoka kabisa, nilinyong’onyea hadi chini nikiwa bila ya msaada. Hali ya usingizi sasa ilinishika. Nusu nikiwa macho, na nusu nimelala, nikawa kama naota ndoto. Juu yangu kabisa na kwa mbali niliuona mji mzuri ambao tunausoma habari zake katika Biblia.  Uzuri wa ajabu kiasi gani jinsi kuta zake za yaspi zilivyokuwa. Niliona mbuga kubwa zilizofunikwa kwa maua zikijitandaza kila upande na kuenea mbali kabisa. Niliona pia mto wa uzima na bahari ya kioo. Makundi makubwa ya malaika waliweza kuingia na kutokea kwenye milango ya mji, wakiimba, eh, nyimbo nzuri kabisa. Kati yao nilimwona mpendwa mama yangu, ambaye alikuwa amekufa miaka michache iliyopita kutokana na kuvunjika moyo, kwa sababu ya uovu wangu. Aliangalia upande wangu na alionekana kuniita kwa kunipungia mkono wake. Lakini sikuweza kuondoka. Ilionekana kuna uzito mkubwa juu yangu mimi ambao ulinikandamiza chini. Sasa upepo mzuri ulipeperusha harufu nzuri ya maua yale ya kupendeza kuelekea kwangu, na niliweza sasa kwa wazi zaidi kuliko wakati mwingine wowote, kusikia wimbo mtamu wa sauti za malaika, na nilisema, eh, laiti ningeweza kuwa mojawapo!

“Nilipokuwa nakunywa kutoka kwenye kikombe hiki cha furaha, ghafla kiliondolewa kwa nguvu kutoka kwenye mdomo wangu. Niliamshwa kutoka kwenye usingizi wangu. Nilirudishwa kutoka kwenye nchi ya furaha niliyokuwa naota na mkaaji wa maskani yangu ya giza, ambaye alisema kwamba wakati ulikuwa umewadia wa kuingia kwenye makao yangu ya baadae. Aliniamuru nimfuate. Nikirudia nyuma niliingia tena kwenye njia ya giza ndani ya mlima na kumfuata kiongozi kwa kitambo, hadi tulipofika kwenye mlango ambao ulifungukia ubavuni mwa njia hii, na nikipitia kwenye mlango huu, tulijikuta hatimaye tunapita kwenye mlango mwingine, na Lo! Niliona Ziwa la Moto.

“Mbele yangu niliweza kuona, kwa kadri ya upeo wa jicho, lile ziwa halisi la moto na kiberiti. Mawimbi makubwa ya moto yaliweza kuvingirika moja juu ya jingine, na mawimbi mengine makubwa ya miali ya moto yakigongana na kuruka juu hewani kama mawimbi ya bahari wakati wa dhoruba kali sana. Kwenye vilele vya mawimbi niliweza kuona binadamu wakinywanyuliwa juu, lakini punde kidogo wakimezwa tena chini hadi kwenye vina vya chini kabisa vya ziwa hili la moto linalotisha. Wakati wakining’inia, kwa muda, juu ya vilele vya mawimbi haya makubwa yatishayo, makufuru yao dhidi ya Mungu wa haki yalikuwa ni ya kutisha, na vilio vya kuhuzunisha kwa ajili ya kuombaomba maji vikawa ni vya kuvunja moyo. Eneo hili kubwa la moto lilisikiwa tena na tena na vilio vya roho hizo zilizopotea.

“Punde kidogo niligeuzwa macho yangu kuelekea kwenye mlango ambao dakika chache kabla niliingilia, na nilisoma maneno haya ya kutisha, ‘Hii ndio hukumu yako; Milele haina mwisho’ Muda kidogo nilianza kuona ardhi ikididimia chini ya miguu yangu, na punde nilijikuta nazama chini kwenye ziwa la moto. Kiu isiyoelezeka kwa ajili ya maji ilinishika sasa. Na nikiitisha maji, macho yangu yalifumbukia kwenye hospitali ya jela.

“Sijawahi hapo nyuma kusimulia hali yangu hii niliyopitia kwa kuogopa kwamba wakuu wa gereza wangeisikia, wangenifikiria mimi ni mwenda wazimu na kunifungia kwenye nyumba ya vichaa. Nilipitia katika hali hii yote, na nimeshawishika kabisa kadri niishivyo hivi kwamba kuna Mbinguni na kuna Jehanamu, Jehanamu ya halisi, aina ile ambayo Biblia huzungumzia. Laki kuna jambo moja la hakika: kamwe siendi mahali pale tena.

“Mara nilipofungua macho yangu hospitalini na kuona kwamba nilikuwa hai na niko duniani kwa mara nyingine, mara moja nilimtolea Mungu moyo wangu na nitaishi na kufa kama Mkristo. Ijapokuwa picha za kuogofya za Jehanamu haziwezi kuondolewa kutoka kwenye kumbukumbu yangu, lakini pia mambo mazuri ya Mbinguni niliyoona siwezi kuyasahau. Nitakwenda kukutana na mpendwa mama yangu baada ya muda. Kuruhusiwa kuketi juu ya kingo za mto ule mzuri, kuzunguka pamoja na wale malaika kati ya mbuga, kupitia kwenye mabonde na juu ya vilima vilivyofunikwa kwa maua yenye harufu tamu, ambao uzuri wake unapita kitu chochote ambacho mwanadamu anaweza kuwazia, kusikiliza nyimbo za waliokombolewa-- hii yote itafidia kwa kuishi kwangu maisha ya Mkristo hapa duniani, hata ingawa nitapaswa kuziacha anasa nyingi za kimwili ambazo nilishirikia kabla ya kuja gerezani. Nimewaacha rafiki zangu nilioshiriki nao katika vitendo vibaya, na nitashirikiana na watu wema wakati nikiwa mtu huru tena.”

Tunatoa maelezo hayo kwa msomaji jinsi tulivyoyapokea kutoka kwa Lennox.

Mungu abariki ujumbe huu kutoka kwa Lennox kwa ajili ya kuzishtua roho nyingine nyingi zilizopotea. Eh, watu wanawezaje kutia shaka ya uwepo wa Jehanamu halisi inayowaka? Tunao Biblia, ambayo ni Neno la Mungu, pamoja na funuo za ajabu kama ya Bwana Lennox, ambazo zote zinafundisha kuhusu Jehanamu isio hadhithi tu. Wanaume  na Wanawake, acha! Ebu ukabili hali halisi! Maisha yako yameandikwa. Mungu anataka kukuokoa na atakusamehe ukiwa tayari kuungama kuwa wewe ni mwenye dhambi. Njia pekee ya wokovu ni kutakaswa kutoka dhambi, kwa kukubali kwamba damu ya Yesu imekuwa sadaka kwa ajili ya dhambi zako. Utakapokubali na msamaha huo wa Mungu, atakupa amani na raha moyoni mwako. Unaweza kuwa huru—huru hapa duniani, na zaidi, utakuwa huru kufurahia fahari za Mbinguni badala ya kuona sio tu masaa arobaini na nane, bali milele katika Jehanamu.

Soma na Luka 16:19-31

Kwa ajili ya Kutolewa Bure – Sio Kuuzwa

Mawasiliano

Kuagiza Vipeperushi

Je, ni Vipi Kuhusu Madawa ya Kulevya, Pombe, na Uzinzi?

Tukabili hali halisi. Maovu ya kutisha - pombe, madawa ya kulevya, na zinaa - vinatishia na kuharibu kile kilichoubwa na Mungu kuwa kizuri. Vinakamata na kuwavuta wadogo kwa wakubwa kama mikono ya pweza mkubwa inavyoshika.

Maambukizo kwa jamii ya leo ni makadirio makubwa. Watu wengi wamelegea bila nanga na kuachwa na laana ya pombe, madawa ya kulevya, na zinaa, wakielekea maangamizi ya milele. Watu wanavutwa upesi na wenzao, pamoja na matangazo yanayotolewa na video, radio, na magazeti kuhusu maovu hayo. Akili inashambuliwa mpaka inachanganyakiwa na kukaa na mawazo ya machafuko ambayo matokeo yake ni uharibifu wa kiroho na kimwili.

Je, akina nani walaumiwe kwa nidhamu na mwenendo wa kuaibisha wa namna hii? Je, ni vijana? Siyo lazima. Kwa kutokumcha Mungu, maisha ya wazazi yamewaidhinishia dhambi ambazo kizazi cha vijana kinapenda. Akina baba na mama hawajui kwamba wanawafundisha watoto wao tabia mbaya ya madawa na ulevi kwa kushindwa kujizuia wenyewe. Kanuni za maadili ya Mungu zimeachwa kwa kutokujali. Kilio cha nguvu kingepanda juu mbinguni. Je, jinsi gani tujiokoe sisi na watoto wetu?

Miji yetu, shule zetu, na vyuo vyetu haziwezi kuzalisha raia katika kiwango kinachofaa kwa mataifa yetu ikiwa matumizi ya dawa za kulevya na pombe huvumiliwa na kuhimizwa kwa uzembe wa wazazi na waalimu.

Matumizi ya pombe ni uharibifu mkubwa wa maadili ya taifa, yakiharibu maamuzi, sifa, na maisha kwa ujumla. Huchangia kuvunjika na kugawanyika kwa familia, ambayo ni mojawapo baraka za Mungu kwa ajili ya wanadamu.

Maandiko kamili ya: Je, ni Vipi Kuhusu Madawa ya Kulevya, Pombe, na Uzinzi?

Zaidi, kuna ongezeko la matumizi ya madawa haramu. Madhara mabaya ya madawa haya ya kulevya ni makubwa zaidi ya faida yao.Utumiaji wa madawa ya kulevya inaweza kusababisha uharibifu wa akili. Watumiaji wa dawa za kulevya wanakubali kwamba hio ni mtego wa mauti: kiakili, kimwili, na kiroho. Uharibifu wa ubongo usiotibika, mauaji, na kujiua ni matokeo mabaya ya anasa hizi.

Kwa sababu ya tabia zao za asili kwa kutamani dhambi, watu wako tayari kufuata mwelekeo na tamaa zinazobuniwa na Shetani. Katika hali hii mwili unataka kuridhishwa pasipo kuzuiliwa. Zinaa hauzimi moto wa tama, bali inachochea. Kuzini siyo uponyaji kwa tamaa, kama vile pombe siyo tiba ya ulevi. Ukweli ni kwamba, tunapaswa kukabili tamaa zetu. Tamaa zinatokea miili yetu ambao itaishia hapa hapa duniani tutakapokufa. Nafsi zetu, yenye kudumu milele, inatamani kuheshimu amri za Mungu.

Uzinzi, Uasherati, Ushoga, Usagaji, na kujamiana na wanyama kumekatazwa na Neno la Mungu. (Walawi 18:23; Wagalatia 5:19-21). Uzinzi huleta maumivu, huzuni, maangamizi, hatia, na magonjwa ya zinaa. Usafi huleta busara ya kujistahifu na heshima. Tusidhani kwamba mtu anayetimiza tamaa zake ndiye mwenye uhuru wala mwenye furaha---hii ni uongo mkubwa. Atendaye dhambi ndiye mtumwa wa dhambi. Mwenye uhuru ndiye anayejikana na kutii sheria ya Mungu.

Wakati watu wametumbukia katika ziwa hilo la tope la ufisadi na upofu wa kiroho, na kuwa na ujasiri wa kutomcha Mungu, Biblia Takatifu imekwisha kujenga msingi ya nidhamu na haki. Bila shaka Biblia ndiyo yenye mamlaka ya milele juu ya masuala ya mema na mabaya. Mungu alimuumba binadamu na haja ya ngono kwa uzazi wa mataifa na kuimarisha au kuboresha kifungo cha ndoa kati ya mume na mke. Aliidhinisha kutimiza haja hii ndani ya ndoa iliyo halali tu. Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu. (Waebrania 13:4).

Mtume Paulo anaandika katika kitabu cha Warumi kuhusu hukumu ya Mungu juu ya kujamiana kijinsia moja (Ushoga/Usagaji). Hivyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu, hata wanawake wakabadili matumizi ya asili kwa matumizi yasiyo ya asili; wanaume nao vivyo hivyo waliyaacha matumizi ya mke ya asili, wakawakiana tamaa, wanaume wakiyatenda yasiyopasa, wakapata nafsini mwao malipo ya upotevu wao yaliyo haki yao. Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa, ambao wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti; wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao. (Warumi 1:26-28,32). Hii ilikuwa ni dhambi ya Sodoma na Gomora iliyochukiza, na Mungu aliwaletea hukumu. (Mwanzo 19). Kulingana na maandiko ni haiwezekani kuwa na Roho Mtakatifu mioyoni mwetu wala kuishi maisha ya Mkristo ikiwa twafanya dhambi hizi.

 Msomaji mpendwa, ili uwe na furaha halisi katika maisha, ili uwe na amani na Mungu, unapaswa kuwa na uhusiano naye. Tambua kwamba wewe ni mwenye dhambi na uungame, na uamini kwamba Yesu alikufa msalabani  akichukua lawama yako. Ushindi unakusubiri!

Unapomfungulia Mungu moyo wako na kuziungama dhambi zako, atakusamehe. Tukizungama dhambi zetu, yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu na kutusafisha na udhalimu wote. (1 Johana 1:9)

Kwa hiari mkabidhi Yesu maisha yako yote kama Mwokozi wako, na ufuate Neno lake pamoja na Roho Mtakatifu kwa utiifu kweli kweli. Baraka zinazopatikana katika maisha  yaliyobadilika ni fikira safi zinazoleta mabadiliko ya ajabu katika matendo yetu na kazi zetu. Kristo atakupa ushujaa kukabili matatizo ya maisha na atakupa nguvu kushindia majaribu ambayo yaweza kukushambulia. Njoo kwa Yesu sasa wakati akikuita. Mtafuteni Bwana madamu anapatikana, mwiteni  madamu yu karibu. (Isaya 55.6)

Mawasiliano

Kuagiza Vipeperushi

Je, Wewe Ni Mwaminifu Kwa Kiasi Gani?

Tazama wapendezwa na kweli iliyo moyoni” (Zaburi 51:6).

Uaminifu ni maadili ya ukweli katika kufungamana na mambo yote ya maisha. Kwa hakika uaminifu ni jambo la moyoni, pia ni fundisho la msingi la Injili ya Yesu Kristo. Mungu anajua mawazo na makusudi ya moyo. Anatambua ukweli kama msingi muhimu kwa maana yeye ni Mungu wa ukweli. (Kumb. 32:4) Hakika atabariki uaminifu uliokamilika wa moyo wetu.

Je, unao tabia ya kusema ukweli wakati ungeweza kupatikana na jambo, lakini ukawa si mwaminifu wakati ambao hakuna atakayekugundua?

Je, kwa makusudi unaweza kumridhisha mtu kwa ushawishi usio wa kweli?

Je, unaweza kufanya manunuzi kwa kukopa wakati ulifahamu kwamba huna uwezo wa kulipa?

Je, unamwambia Mungu jinsi mambo yalivyo wakati unapomwomba?

Je, kwa uaminifu unalitenda kila jambo ambalo unafahamu Mungu anakutaka ulitende?

Maandiko kamili ya: Je, Wewe Ni Mwaminifu Kwa Kiasi Gani?

Je, wewe ni mwaminifu kuhusu mafundisho ya Biblia?

Je, jinsi unavyojifanya kuonekana, kweli ndivyo ulivyo?

Kuna hadithi ya kuchochea hisia katika Agano Jipya ya mtu aitwaye Anania na mkewe Safira katika kitabu cha Matendo 5:1-11. Waliuza mali yao kama wengine nao walivyofanya na kujifanya kutoa fungu lote kwa kanisa, wakati kwa hila walikubaliana kubakiza sehemu ya malipo kwa ajili yao. Anania na Safira walileta pesa hizi mbele ya viongozi wa kanisa wakisema kwamba waliuza shamba hilo kwa kiasi hicho walicholeta. Udanganyifu wao ulihukumiwa na Mungu mara moja na kuadhibishwa kwa kifo. Katika habari hii ya kanisa la mwanzo, unafiki (au udanganyifu) ulikuwa ukiadhibishwa kwa ukali. Mungu hapuuzi uzushi huu. Nasi kama Anania na Safira huenda tunaweza tukatoa uzushi unaoridhisha hata kama maneno tuyasemayo siyo ya uongo. Twaelekea kusahau uwajibikaji wetu mbele za Mungu. Mungu ajua jinsi mioyo yetu ilivyo, na anatutegemea tuwe waaminifu na wa kwelikweli.

Mnafiki hujifanya kuwa mtu ambaye siye yeye. Huenda anadai kuwa mwaminifu, lakini wakati ambao ingekuwa manufaa kwake, yuko tayari kusema uongo. Labda anaweza kuzungumzia vizuri kuhusu mahitaji ya wasiobahatika, lakini siye mkarimu wa kutoa muda wala msaada wakati maafa au matatizo yakitokea. Mtu mwingine aweza kujifanya kuwa mkarimu kujishughulisha na mambo ya majirani zake, na bado akatumia fursa hio kuwasengenya. Mwingine huenda anajionyesha kuwa mtu mnyofu, lakini bado yuko tayari kuchukua pesa za mtu mwingine, maadamu asigunduliwe katika tendo hilo. Huenda atajaribu kujiaminisha binafsi  kwamba anaishi maisha ya juu kitabia kuliko watu wengine wakati yeye ni mdanganyifu. Mtu aliye na tabia hizi ni mnafiki wala si mwaminifu.

Unafiki wa wanadamu kila wakati ni kitu cha kumhuzunisha Mungu. Yesu asema, “Watu hawa huniheshimu kwa midomo; Ila mioyo yao iko mbali nami” (Mathayo 15:8). Changamoto kubwa kwa mwanadamu ni kuweka mdomo na moyo kwa pamoja. Uaminifu kutoka ndani yetu ndio ufunguo wa kupata neema na fadhili kwa Bwana.

Mkristo wa kweli ni mfano wa uaminifu. Kustawi kwake kiroho huendana na unyofu wake mbele ya Mungu. Uaminifu kwa binadamu wenzetu pia ni muhimu na unahitaji usikivu wa umakini. Katika maneno yetu, matendo ya shughuli zetu, na hata makubaliano ya kibiashara ni lazima tuhifadhi imani kwa watu wote. Ili tutende hili, ni lazima tuwe tayari kupata hasara kwa ajili ya ukweli.

Kuna somo tunaloweza kujifunza kutokana na simulizi hii. Mwalimu alimwuliza kijana mmoja swali:

“Je, ungesema uongo ukilipwa shilingi 50?”

“La hasha, mama” kijana akamjibu.

“Je, ungeweza kusema uongo ukilipwa shilingi elfu mbili?”

“La hasha, mama” kijana akamjibu.

“Je, ungeweza kusema uongo ukilipwa shilingi milioni mbili?”

“Lo!” akajisemea moyoni. “Ni kitu gani nisichoweza kukifanya nikiwa na shilingi milioni mbili?”

Wakati akisitasita, kijana mwingine nyuma yake akasema, “La hasha, mama”.

“Ni kwa nini?” mwalimu akauliza.

“Kwa sababu uongo unashikamana na mtu. Wakati hio hela zitakapoisha, na vitu vyote vizuri vilivyonunuliwa na pesa hizo vimetoweka, UONGO utabakia pale pale ulipo.”

Ukweli una umuhimu kiasi kwamba tungekuwa tayari kusumbukiwa kwa ajili yake. Sisi tukiwa tayari kusema uongo ili tujiokoe kutoka kwa kuaibishwa kwa muda mfupi, ni gharama kubwa mno kulipa kwa ajili ya kupotewa na uadilifu wetu. Pesa zipatikanazo kwa njia ya ujanja ni malipo duni kwa kujipatia dhamiri iliyonajisika, na hukumu ya milele ya Mungu inayokuja.

Je, wasema kwamba unatembea katika nuru ya Mungu na wakati huo huo unayatenda matendo maovu kama:

  • Unakataa kumsamehe ndugu au dada yako?
  • Hufanyi mapatano unapomtendea mtu vibaya?
  • Unatia chumvi kwenye ukweli?
  • Unavunja ahadi zako?
  • Unamwibia Mungu sadaka na zaka zake?
     

Uaminifu ni mtihani wa moyo. Mungu anafahamu mioyo yetu, na hakuna kitu kilichositirika kwake. Walakini wakati mwingine hatuwezi kumwambia Mungu kwa kadiri anavyotujua na jinsi tunavyojihisi ndani mwetu. Huenda hatuwaonyeshi jinsi ndivyo tulivyo kwa watu wengine. Mtu wa kweli mwenye furaha ni yule aliye mwaminifu mbele za Mungu, na anajikubali na kukiri jinsi alivyo. Na tukifungua mioyo na maisha yetu kwa Mungu, matatizo haya yote yanatatuliwa.

Malengo na misimamo yetu yanahitaji kuwasilishwa kwenye kipimo cha uaminifu. Kufaulu mtihani huu katika matendo yetu kwa Mungu na wanadamu, twahitaji mabadiliko ya ndani ya moyo, kwa maana mambo ya nje yanafafanua utu wetu wa ndani. Je, wewe ni mwaminifu? Mungu anatudai unyofu, watu wengine wote wanautegemea, na sisi wenyewe tutanufaika kwa kuushika. Ndiyo maisha yaliyo na thamani. “Tuna hakika kuwa tunayo dhamiri safi na shauku ya kuishi kwa uadilifu kwa kila njia.” (Waebrania 13:18 Tafsiri la NENO). Soma pia Mambo ya Walawi 19:35-36 na Mithali 19:5.

Mawasiliano

Kuagiza Vipeperushi