Yesu Kristo Atakuja Tena

Bwana Yesu alikuja ulimwenguni kuwaokoa wanadamu kutoka kwa dhambi zao. “Bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa akawa ana mfano wa wanadamu” (Wafilipi 2:7). Alikufa kwa ajili ya dhambi za watu wote ulimwenguni, alizikwa  na akafufuka tena (1Wakorintho 15:4), kisha akapaa kwenda mbinguni tena (Matendo 1:9). Mitume walimwona na pia waumini zaidi ya mia tano, baada ya kufufuka. Baada ya kupaa kwenda mbinguni, malaika wawili waliwaambia mitume kwamba kurudi kwake kutafanana na kupaa kwake. Ni Mungu tu ndiye anayefahamu ni lini Bwana atarudi. Huenda itakuwa ni jioni au usiku wa manane, au wakati wa asubuhi au alasiri. (Marko 13:35) “Kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari; kwa kuwa katika saa msiyodhani Mwana wa Adamu yuaja” (Mathayo 24:44).

Baadhi wametabiri wakati wa kurudi kwake, hadi siku na saa. “Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila baba peke yake” (Mathayo 24:36).  Atakuja haraka kama vile umeme utokavyo mashariki hadi magharibi (Mathayo 24:27). Atakuja wakati tusiotarajia kama mwizi anavyokuja usiku (2Petro 3:10). Siku hio itawajia kwa ghafla, kama mtego unasavyo (Luka 21:34). Bwana, katika hekima isiyo na vikomo, atarudi kumlipa kila mtu sawasawa na alivyotenda (Ufunuo 22:12). “Na hilo niwaambialo ninyi, nawaambia wote, kesheni” (Marko 13:37).

Dalili za Nyakati na za Kurudi Kwake

Bwana ameeleza dalili ambazo kwazo tuweze kutambua kwamba kurudi kwake kumekaribia. “Basi, kwa mtini jifunzeni mfano; tawi lake likiisha kuchipuka na kuchanua majani, mwatambua ya kuwa wakati wa mavuno u karibu: Nanyi kadhalika, myaonapo hayo yote, tambueni ya kuwa u karibu, milangoni” (Mathayo 24:32-33). Kutakuweko:

  • Vita na matetesi ya vita (Mathayo 24:6)
  • Taifa litaondoka kupigana na taifa (Mathayo 24:7)
  • Matetemeko ya nchi, njaa na tauni (Mathayo 24:7)
  • Uovu utaongezeka, upendo utapoa (Mathayo 24:12)
  • Makristo na waalimu wa uongo (Mathayo 24:11, 24; Marko 13:22)
  • Siku kama wakati wa Nuhu (Mathayo 24:37)
  • Ishara katika jua, mwezi na nyota (Luka 21:25)
  • Mshangao wa mataifa na msukosuko (Luka 21:25)
  • Watu wakivunjika mioyo kwa hofu (Luka 21:26)
  • Watu wakisema amani na usalama (1Wathesalonike 5:3)
  • Nyakati za hatari (2Timotheo 3:1-5)
  • Wapendao anasa na wenye mfano wa utauwa (2Timotheo 3:1-7)
  • Watu waovu wakizidi kuwa waovu (2Timotheo 3:13)
  • Ukengeufu (Uasi) (2Wathesalonike 2:3)
  • Kujiweka akiba kwa ajili ya tamaa za kimwili (Yakobo 5:1-15)
  • Wenye kufanya dhihaka (2Petro 3:3-10)
  • Watu wenye kudhihaki wafuatao tamaa zao (Yuda 16, 17, 18)

Siku hizi asilimia kubwa ya dalili hizi zimedhihirishwa tayari. Uzinzi, uasherati, kuvunjika kwa ndoa na kuoana na mwingine, ushoga, uhalifu, na maovu yanaongezeka kwa haraka na kutapakaa kwa mapana. Hayo yote na dhambi zingine zinaharakisha kurudi kwa Bwana. Mambo haya yameandikwa “mpate kuyakumbuka yale maneno yaliyonenwa zamani na manabii watakatifu, na ile amri ya Bwana na Mwokozi iliyoletwa na mitume wenu” (2Petro 3:2). Watenda dhambi wataogopa kuona ujio wake, lakini watakatifu wataushangilia.

Maandiko kamili ya: Yesu Kristo Atakuja Tena

JE, UKO TAYARI? Unayo amani na Mungu na wanadamu wenzako? Je, kuna jambo lo lote katika maisha yako linalokuzuia kusema, “Amina; na uje, Bwana Yesu” (Ufunuo 22:20)?

 

Mawasiliano

Kuagiza Vipeperushi

Je, ni Vipi Kuhusu Madawa ya Kulevya, Pombe, na Uzinzi?

Tukabili hali halisi. Maovu ya kutisha - pombe, madawa ya kulevya, na zinaa - vinatishia na kuharibu kile kilichoubwa na Mungu kuwa kizuri. Vinakamata na kuwavuta wadogo kwa wakubwa kama mikono ya pweza mkubwa inavyoshika.

Maambukizo kwa jamii ya leo ni makadirio makubwa. Watu wengi wamelegea bila nanga na kuachwa na laana ya pombe, madawa ya kulevya, na zinaa, wakielekea maangamizi ya milele. Watu wanavutwa upesi na wenzao, pamoja na matangazo yanayotolewa na video, radio, na magazeti kuhusu maovu hayo. Akili inashambuliwa mpaka inachanganyakiwa na kukaa na mawazo ya machafuko ambayo matokeo yake ni uharibifu wa kiroho na kimwili.

Je, akina nani walaumiwe kwa nidhamu na mwenendo wa kuaibisha wa namna hii? Je, ni vijana? Siyo lazima. Kwa kutokumcha Mungu, maisha ya wazazi yamewaidhinishia dhambi ambazo kizazi cha vijana kinapenda. Akina baba na mama hawajui kwamba wanawafundisha watoto wao tabia mbaya ya madawa na ulevi kwa kushindwa kujizuia wenyewe. Kanuni za maadili ya Mungu zimeachwa kwa kutokujali. Kilio cha nguvu kingepanda juu mbinguni. Je, jinsi gani tujiokoe sisi na watoto wetu?

Miji yetu, shule zetu, na vyuo vyetu haziwezi kuzalisha raia katika kiwango kinachofaa kwa mataifa yetu ikiwa matumizi ya dawa za kulevya na pombe huvumiliwa na kuhimizwa kwa uzembe wa wazazi na waalimu.

Matumizi ya pombe ni uharibifu mkubwa wa maadili ya taifa, yakiharibu maamuzi, sifa, na maisha kwa ujumla. Huchangia kuvunjika na kugawanyika kwa familia, ambayo ni mojawapo baraka za Mungu kwa ajili ya wanadamu.

Maandiko kamili ya: Je, ni Vipi Kuhusu Madawa ya Kulevya, Pombe, na Uzinzi?

Zaidi, kuna ongezeko la matumizi ya madawa haramu. Madhara mabaya ya madawa haya ya kulevya ni makubwa zaidi ya faida yao.Utumiaji wa madawa ya kulevya inaweza kusababisha uharibifu wa akili. Watumiaji wa dawa za kulevya wanakubali kwamba hio ni mtego wa mauti: kiakili, kimwili, na kiroho. Uharibifu wa ubongo usiotibika, mauaji, na kujiua ni matokeo mabaya ya anasa hizi.

Kwa sababu ya tabia zao za asili kwa kutamani dhambi, watu wako tayari kufuata mwelekeo na tamaa zinazobuniwa na Shetani. Katika hali hii mwili unataka kuridhishwa pasipo kuzuiliwa. Zinaa hauzimi moto wa tama, bali inachochea. Kuzini siyo uponyaji kwa tamaa, kama vile pombe siyo tiba ya ulevi. Ukweli ni kwamba, tunapaswa kukabili tamaa zetu. Tamaa zinatokea miili yetu ambao itaishia hapa hapa duniani tutakapokufa. Nafsi zetu, yenye kudumu milele, inatamani kuheshimu amri za Mungu.

Uzinzi, Uasherati, Ushoga, Usagaji, na kujamiana na wanyama kumekatazwa na Neno la Mungu. (Walawi 18:23; Wagalatia 5:19-21). Uzinzi huleta maumivu, huzuni, maangamizi, hatia, na magonjwa ya zinaa. Usafi huleta busara ya kujistahifu na heshima. Tusidhani kwamba mtu anayetimiza tamaa zake ndiye mwenye uhuru wala mwenye furaha---hii ni uongo mkubwa. Atendaye dhambi ndiye mtumwa wa dhambi. Mwenye uhuru ndiye anayejikana na kutii sheria ya Mungu.

Wakati watu wametumbukia katika ziwa hilo la tope la ufisadi na upofu wa kiroho, na kuwa na ujasiri wa kutomcha Mungu, Biblia Takatifu imekwisha kujenga msingi ya nidhamu na haki. Bila shaka Biblia ndiyo yenye mamlaka ya milele juu ya masuala ya mema na mabaya. Mungu alimuumba binadamu na haja ya ngono kwa uzazi wa mataifa na kuimarisha au kuboresha kifungo cha ndoa kati ya mume na mke. Aliidhinisha kutimiza haja hii ndani ya ndoa iliyo halali tu. Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu. (Waebrania 13:4).

Mtume Paulo anaandika katika kitabu cha Warumi kuhusu hukumu ya Mungu juu ya kujamiana kijinsia moja (Ushoga/Usagaji). Hivyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu, hata wanawake wakabadili matumizi ya asili kwa matumizi yasiyo ya asili; wanaume nao vivyo hivyo waliyaacha matumizi ya mke ya asili, wakawakiana tamaa, wanaume wakiyatenda yasiyopasa, wakapata nafsini mwao malipo ya upotevu wao yaliyo haki yao. Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa, ambao wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti; wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao. (Warumi 1:26-28,32). Hii ilikuwa ni dhambi ya Sodoma na Gomora iliyochukiza, na Mungu aliwaletea hukumu. (Mwanzo 19). Kulingana na maandiko ni haiwezekani kuwa na Roho Mtakatifu mioyoni mwetu wala kuishi maisha ya Mkristo ikiwa twafanya dhambi hizi.

 Msomaji mpendwa, ili uwe na furaha halisi katika maisha, ili uwe na amani na Mungu, unapaswa kuwa na uhusiano naye. Tambua kwamba wewe ni mwenye dhambi na uungame, na uamini kwamba Yesu alikufa msalabani  akichukua lawama yako. Ushindi unakusubiri!

Unapomfungulia Mungu moyo wako na kuziungama dhambi zako, atakusamehe. Tukizungama dhambi zetu, yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu na kutusafisha na udhalimu wote. (1 Johana 1:9)

Kwa hiari mkabidhi Yesu maisha yako yote kama Mwokozi wako, na ufuate Neno lake pamoja na Roho Mtakatifu kwa utiifu kweli kweli. Baraka zinazopatikana katika maisha  yaliyobadilika ni fikira safi zinazoleta mabadiliko ya ajabu katika matendo yetu na kazi zetu. Kristo atakupa ushujaa kukabili matatizo ya maisha na atakupa nguvu kushindia majaribu ambayo yaweza kukushambulia. Njoo kwa Yesu sasa wakati akikuita. Mtafuteni Bwana madamu anapatikana, mwiteni  madamu yu karibu. (Isaya 55.6)

Mawasiliano

Kuagiza Vipeperushi

Hamna Budi Kuzaliwa Mara ya Pili

Yesu anatuambia kwamba milango ya mbinguni imefungwa dhidi yetu isipokuwa tunazaliwa mara ya pili. Kwa hiyo twauliza: “Rafiki, umezaliwa mara ya pili?” “Muumini wa kanisa, umezaliwa mara ya pili?” Ikiwa hapana, basi umepotea. Kwa maana Yesu anasema, “Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu” (Yohana 3:3). Kwa kweli hakuna mtu anayetaka kufa akiwa mwenye dhambi, au kupotea; basi hamna budi kuzaliwa mara ya pili.

Unaweza ukauliza, “Kuzaliwa mara ya pili maana yake ni nini?” Leo, kuna mafundisho mengi ya uongo kuhusu kuzaliwa mara ya pili. Siyo ubatizo, kwa kuwa wengine walibatizwa na bado hawajazaliwa mara ya pili (Matendo 8:9-25). Siyo kujiunga na kanisa, kwa sababu wengine waliingia ndani kwa siri bila kufahamika (Wagalatia 2:4). Siyo kula meza ya Bwana, kwa maana baadhi walikula isiyostahili na iliwaletea hukumu (1Wakorintho 11:29). Siyo kubadilika au kujaribu kuishi maisha bora, “kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze” (Luka 13:24). Siyo kusali, kwa maana Yesu asema, “Watu hawa huniheshimu kwa midomo; ila mioyo yao iko mbali nami” (Mathayo 15:8).

Mtu mwingine anaweza akasema, “Nikijaribu kuyafanya yote niwezayo: kuwapa maskini, kuwatembelea wagonjwa na kuwa mwema kila siku kadiri niwezavyo, basi kwa kweli nimezaliwa mara ya pili.” La, hasha, hatuwezi kuwa tofauti na jinsi tulivyo moyoni. “Kwa kuwa ile nia ya mwili ni uadui juu ya Mungu, kwa maana haitii sheria ya Mungu wala haiwezi kuitii” (Warumi 8:7). “Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri.” (Mathayo 7:18) Tunapaswa kuwa na moyo uliobadilika. Kwa kuwa Mungu kupitia manabii, asema hivi, “Nami nitawapa ninyi moyo mpya, nami nitatia roho mpya ndani yenu, nami nitatoa moyo wa jiwe uliomo ndani ya mwili wenu, nami nitawapa moyo wa nyama” (Ezekieli 36:26).

Hivyo basi, kuzaliwa upya maana yake nini?” Kiini cha kuzaliwa upya ni kuwa na mabadiliko ya moyo kutoka kwa maisha ya kujitumikia kibinafsi, na kupata maisha ya kumtumikia Bwana. Mabadiliko haya hutokea wakati tunapojutia dhambi zetu, na kwa imani tukamtazamia Yesu kwa kuomba msamaha. Mtoto azaliwapo, uhai mpya unatokea, binadamu mpya katika mwili. Hali kadhalika, tunapozaliwa upya kwa roho, uhai mpya huu hutokea ambao ni ndani ya Yesu Kristo na unaongozwa na Roho Mtakatifu. Hivyo basi, kunaitwa kuzaliwa: uhai mpya ndani ya Kristo Yesu. “Bwana hakawii kuitimiza ahadi yaki, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba (2Petro 3:9).

Maandiko kamili ya: Hamna Budi Kuzaliwa Mara ya Pili

“Ni lini nitegemee kuzaliwa mara ya pili?” Maandiko matakatifu yasema, “Leo, kama mtaisikia sauti yake,” (Waebrania 3:7). Hii inamaanisha kwamba katika umri wowote, wakati wowote, au mahali popote, ukisikia mwito wake na kuitika unaweza ukazaliwa kwa mara ya pili kwa njia ya Roho.

“Itachukua muda gani? Si nitakua taratibu katika kuzaliwa upya?” La, tunazaliwa kwanza katika ufalme wa Mungu na kunatufanya tuwe wana na warithi. “na kama tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo” (Warumi 8:17). Kuzaliwa mara ya pili kunaweza kutokea mara moja unapomtolea Yesu vyote na kumwendea kupata msamaha.

“Kwa njia gani na lini ninaweza kuupokea?” Mungu anayechunguza moyo, aona uaminifu wako. Anakujia kupitia nguvu ya Roho Mtakatifu, na kuumbia moyoni mwako roho wa kweli. (Zaburi 51:10) Kwa njia hii unazaliwa upya- kiumbe kipya katika Kristo Yesu kwa kuwa na imani kwake. (2Wakorintho 5:17).

Hatimaye: “Kwa jinsi gani naweza kufahamu kwamba nimezaliwa upya tayari?” Paulo katika Warumi 8:1-10 anafundisha; “Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo sio wake”. Biblia yafundisha kwamba waliopotea wamekufa dhambini, wamelaaniwa, na wana dhamiri iliyo ya uovu. Wana mawazo yenye tamaa ya kimwili, wasio na tumaini, wasiotii, na wasio na Mungu ulimwenguni. Lakini Mkristo aliyezaliwa mara ya pili ni mtoto wa Mungu, yu hai katika Kristo, ameokolewa, hana hatia ya dhambi, na anayo dhamiri safi. Naye anayo nia ya kiroho, amejazwa na Roho Mtakatifu na imani, na analo tumaini la uzima wa milele. Dhambi zake zimeondolewa kwa damu ya Yesu Kristo. Moyo wake umejazwa na upendo na amani wa Mungu zinazozidi ufahamu wote. Anayapenda mapenzi ya Bwana, na anayo shauku na amepewa uwezo kuyafanya mapenzi hayo. Pia anatembea na tumaini la uzima ng’ambo ya kaburi, na anayo ahadi ya makao yaliyopo mbinguni. Je, mtu anaweza kupata mageuzi kama haya na asiyatambue? La, hasha kwani “Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu” (Warumi 8:16). Ikiwa hujapata mabadiliko haya yaletayo amani na furaha moyoni, usipuuze, mtafute Mungu kwa moyo mmoja; kwa kuwa ni roho yako mwenyewe. Ni lazima uzaliwe mara ya pili.

Mawasiliano

Kuagiza Vipeperushi